• Malalamiko |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
Bunda District Council
Bunda District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji & Ushirika
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maji
      • Fedha & Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Mifugo & Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi & Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Elimu Msingi
    • Barabara
    • Mifugo
    • Afya
    • Mazao ya kilimo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi & Mipango
      • Elimu, Afya & Maji
      • AIDS Control
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Uma
    • Video
    • Hifadhi ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WENYEVITI WA VIJIJI NA MTAA MARUFUKU KUMILIKI MUHURI.

Posted on: March 21st, 2025



Katika kikao cha mkutano wa Halmashauri kuu ya Chama cha mapinduzi (CCM), Wilaya ya Bunda kilichofanyika siku ya tarehe 20/3/2025 katika ukumbi wa Malaika, Mkuu wa Wilaya ya Bunda Mh. Aswege Enock Kaminyoge alisoma waraka wenye muongozo unaokataza wenyeviti wa vijiji na mitaa kumiliki muhuri.


Lengo la kusoma waraka huo ni baada ya wenyeviti wa vijiji na mitaa kuomba kumiliki muhuri hiyo kama kitendea kazi chao, kitu ambacho Mkuu wa Wilaya ilibidi kusoma waraka huo ambao umeelezea na kutolea ufafanuzi kwanini hawapaswi kuwa nao na vifaa ambavyo wanatakiwa kuwa navyo kama sehemu ya vitendea kazi.


Mh.Kaminyoge alisema wajibu wa mwenyekiti wa MTAA na Kijiji ni kusimamia, kuhamasisha, kufuatilia, kuongoza, kuwasilisha, kushirikisha, kusuluhisha, kuhifadhi na kudumisha amani katika MTAA au kijiji anachoongoza.


Muongozo wa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali mitaa wenye kumb. Na. CCB.126/215/01 wa tarehe 30/11/2016 unaelezea matumizi ya mihuri kwa wenyeviti wa mitaa na vijiji kwamba wanatakiwa kuacha mara Moja kutumia mihuri katika majukumu ya kiutendaji na badala yake uwekaji au ugongaji wa mihuri ufanywe na maafisa watendaji wa eneo husika.


Pale ambapo MTAA au kijiji hakuna Mtendaji wa MTAA au kijiji, mwenyekiti wa MTAA au kijiji amtambulishe Mwananchi mwenye kuhitaji huduma ya kugongewa muhuri kwa Mtendaji wa kata ili aweze kugongewa muhuri wa kata.


Hivyo basi, kwa mujibu wa taratibu za kazi za mwenyekiti wa MTAA na Kijiji aliyechaguliwa na wananchi anatakiwa kuwa au kumiliki vifaa vifuatavyo ambavyo ni bendera yenye nembo ya Halmashauri, rejista ya wakazi wa MTAA au kijiji na daftari la mihtasari ya vikao vya MTAA au kijiji.


Mh. Kaminyoge aliwaagiza Wakurugenzi watendaji wa Halmashauri kuhakikisha wanasimamia utekelezaji wa maelekezo haya ili kuweza kuepusha migogoro isiyokuwa ya lazima katika mitaa na vijiji.


" Watendaji wa mitaa na vijiji watakaobainika kutumia mihuri vibaya na kuendeleza migogoro hususani ya ardhi watachukuliwa hatua Kali za kisheria." Alisema Mkuu wa Wilaya.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI June 04, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI September 18, 2024
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WOTE December 20, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRATIBU WA MRADI WA BCRAP ATAJA VIPAUMBELE VITAKAVYOENDA KUTEKLELEZWA KWA AWAMU YA PILI YA MRADI

    June 11, 2025
  • ZAIDI YA MILIONI 300 ZA POKELEWA KATIKA UTEKELEZAJI WA MRADI WA KUHIMILI ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIA NCHI

    June 09, 2025
  • ELIMU YA UTUNZAJI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA YATOLEWA KWA WANAFUNZI WA SHULE YA SEKONDARI MWIBARA

    June 04, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    June 03, 2025
  • Angalia zote

Video

Mvamizi wa eneo la soko.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Dira na Dhamira
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Mpango Mkakati
  • Mpango wa Uwekezaji Sekta ya Samaki
  • Muundo wa Taasisi
  • OPRAS - Form

Viunganishi Muambata

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2023 Bundadc
  • Matokeo ya darasa la saba
  • Matokeo ya darasa la saba
  • PO-RALG
  • PO-PSM
  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2019

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Kibara Stoo.

    Anuani ya Posta: 126, Bunda

    Simu: 0282621055

    Hamishika:

    Barua Pepe: ded@bundadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki@ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bunda