Katika kuelekea kilele cha maadhimisho ya siku ya mazingira Duniani, Halmashauri ya Wilaya ya Bunda kupitia kitengo cha Maliasili na uhifadhi wa mazingira kimeendelea kufanya shughuli mbalimbali za utunzaji wa mazingira ikiwemo shughuli za upandaji miti shuleni, na utoaji wa elimu kwa wanafunzi namna ya utunzaji na umuhimu wa usafi wa mazingira yanayowazunguka.
Afisa Mazingira wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda Bi.Elivaileth Liampawe siku ya tarehe 4/6/2025 ametoa elimu ya namna ya utunzaji wa mazingira kwa wanafunzi wa shule ya Sekondari Mwibara, ambapo wamefundishwa maana ya mazingira na hasara zinazosababishwa na magugu vamizi katika miti mbalimbali.
Hivyo, wanafunzi wamefanya zoezi la kuhakikisha wanayaondoa magugu vamizi yote yaliyokuwa yametapakaa kwenye miti.
Siku ya mazingira Duniani huadhimishwa Kila ifikapo tarehe 5/6 ya Kila mwaka, mwaka huu siku ya mazingira Duniani imebeba kauli mbiu isemayo:
" MAZINGIRA YETU NA TANZANIA IJAYO TUWAJIBIKE SASA, DHIBITI MATUMIZI YA PLASTIKI".
Kibara Stoo.
Anuani ya Posta: 126, Bunda
Simu: 0282621055
Hamishika:
Barua Pepe: ded@bundadc.go.tz
Haki Miliki@ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bunda