• Malalamiko |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
Bunda District Council
Bunda District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji & Ushirika
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maji
      • Fedha & Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Mifugo & Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi & Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Elimu Msingi
    • Barabara
    • Mifugo
    • Afya
    • Mazao ya kilimo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi & Mipango
      • Elimu, Afya & Maji
      • AIDS Control
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Uma
    • Video
    • Hifadhi ya Picha
    • Habari
    • Matukio

ELIMU YATOLEWA KWA WAJUMBE WA MABARAZA YA KATA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA

Posted on: July 10th, 2025



Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, kupitia kitengo cha huduma za Sheria siku ya tarehe 9/7/2025 kiliwajengea uwezo wa namna ya kusuluhisha migogoro ya ardhi katika Kata.


Mkuu wa kitengo cha huduma za Sheria wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, Bi. Scola Kisibo aliwasomea mwongozo wa usuluhishi wa migogoro ya ardhi katika mabaraza ya kata, ambapo, alisema kazi ya mabaraza ya kata ni kusuluhisha tu na sio kutoa hukumu katika malalamiko yatakayowasilishwa kuhusiana na migogoro ya ardhi katika Kata, pia, alisema migogoro hiyo ni lazima iwe ndani ya kata husika na ihusishe mlalamikaji na mlalamikiwa katika uwasilishwaji wa malalamiko hayo.


Aliwasomea sifa za kuwa mjumbe wa Baraza la kata, na kusema muda wa kuhudumu ndani ya Baraza la kata ni miaka mitatu, na baada ya hapo watachagua wajumbe wengine wapya au kuwarudisha watakaokuwa na sifa.


" Mtu hatachaguliwa kuwa mjumbe wa Baraza la kata endapo atakosa sifa hizi:, kama sio raia wa Tanzania, akiwa na umri wa chini ya miaka 18, akiwa Mtumishi wa umma, au akiwa mjumbe wa Baraza la ardhi la Kijiji, Halmashauri ya Kijiji au kamati ya Maendeleo ya kata, mwanasheria au mtu yeyote aliyeajiriwa na mahakama, Mbunge, au kama amewahi kutiwa hatiani kwa kosa lolote la jinai." Alisema Bi. Kisibo.


Mwanasheria aliwasomea mambo muhimu yanayotakiwa kuzingatiwa katika mabaraza hayo wakati wa usuluhishi na hatua za kufuata katika usuluhishi.



Wajumbe walishukuru na kupongeza kitengo cha Sheria kwa kuweza kuwajengea uwezo katika usimamizi na uendeshaji wa mabaraza ya kata hususani katika usuluhishi wa migogoro ya ardhi ndani ya kata, kwani itawasaidia kutatua migogoro itakayokuwa inajitokeza ndani ya kata zao mapema zaidi.


Mafunzo ya wajumbe wa mabaraza ya kata yalitolewa katika Kata ya Nyamuswa na Nyamang'uta, katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI June 23, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI September 18, 2024
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WOTE December 20, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ELIMU YATOLEWA KWA WAJUMBE WA MABARAZA YA KATA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA

    July 10, 2025
  • WAWAKILISHI WA WAZEE WAKUTANA KWA AJILI YA KUSOMEWA MUONGOZO MPYA WA UANZISHWAJI WA BARAZA LA WAZEE KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA

    July 04, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA YATAKIWA KUTOA ELIMU KWA WAFANYABIASHARA KUHUSIANA NA UUZAJI NA UNUNUZI WA KUTUMIA STAKABADHI GHALANI

    July 02, 2025
  • ZIARA YA MKURUGENZI MTENDAJI YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MAENDELEO YA UJENZI KATIKA HOSPITALI YA WILAYA

    June 27, 2025
  • Angalia zote

Video

Mvamizi wa eneo la soko.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Dira na Dhamira
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Mpango Mkakati
  • Mpango wa Uwekezaji Sekta ya Samaki
  • Muundo wa Taasisi
  • OPRAS - Form

Viunganishi Muambata

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2023 Bundadc
  • Matokeo ya darasa la saba
  • Matokeo ya darasa la saba
  • PO-RALG
  • PO-PSM
  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2019

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Kibara Stoo.

    Anuani ya Posta: 126, Bunda

    Simu: 0282621055

    Hamishika:

    Barua Pepe: ded@bundadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki@ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bunda