• Malalamiko |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
Bunda District Council
Bunda District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji & Ushirika
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maji
      • Fedha & Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Mifugo & Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi & Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Elimu Msingi
    • Barabara
    • Mifugo
    • Afya
    • Mazao ya kilimo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi & Mipango
      • Elimu, Afya & Maji
      • AIDS Control
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Uma
    • Video
    • Hifadhi ya Picha
    • Habari
    • Matukio

HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA YATAKIWA KUTOA ELIMU KWA WAFANYABIASHARA KUHUSIANA NA UUZAJI NA UNUNUZI WA KUTUMIA STAKABADHI GHALANI

Posted on: July 2nd, 2025



Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Mh. Aswege Enock Kaminyoge siku ya tarehe 1/7/2025 alifungua kikao cha Baraza la wafanyabiashara, kilichofanyika katika ukumbi wa mkutano wa Halmashauri ya Mji wa Bunda.

Kikao hicho,kilihudhuriwa na wafanyabiashara mbalimbali kutoka katika Wilaya ya Bunda, wakuu wa taasisi za umma na binafsi, wakuu wa divisheni na vitengo kutoka Halmashauri zote mbili, pamoja na kamati ya usalama ya Wilaya.


Lengo la kuitisha kikao hicho ni kuelezea fursa mbalimbali za uwekezaji zinazopatikana katika Wilaya ya Bunda,ambapo wafanyabiashara walielezea changamoto wanazokabiliana nazo katika uwekezaji wao ikiwemo kutokuwa na elimu ya kutosha kuhusiana na mfumo wa uuzaji na ununuzi wa mazao kupitia stakabadhi ghalani.


Kutokana na kutokuwa na elimu hiyo wameshindwa kuelewa ni namna Gani mfumo huo unavyowanufaisha wakulima katika uuzaji wa mazao yao baada ya kuvuna kutoka shambani.


Changamoto nyingine waliyobainisha ni kutokutangazwa kwa sekta za utalii katika Wilaya ambapo walisema kama wangepata elimu ya kutosha katika sekta hizo muhimu wawekezaji wengi wangeweza kunufaika nazo.


Mh.Kaminyoge alimuagiza Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda , Ndugu Stafa Nashon kuhakikisha wanaenda kuitisha kikao cha wafanyabiashara wote na AMCOS zote zilizopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda na kuhakikisha wanawapa elimu ya kutosha juu ya mfumo wa uuzaji na ununuaji wa mazao kupitia stakabadhi ghalani kabla ya msimu mwingine wa mnada wa uuzaji wa mazao hayo haujaanza.

" Halmashauri zote mbili zihakikishe zinatumia tovuti na mitandao ya kijamii kuhakikisha wanatoa elimu na matangazo ya fursa za uwekezaji ndani ya Wilaya." Alisema.


Naye, Meneja wa TRA Wilaya aliwashukuru na kuwapongeza, wafanyabiashara wote wa Bunda kwa kuweza kulipia Kodi kwa wakati hadi kupelekea mamlaka ya Kodi Wilaya ya Bunda kuvuka lengo kwa mwaka wa fedha 2024/2025, ambapo mamlaka iliweka lengo la kukusanya Tshs Million 810, lakini kutokana na wafanyabiashara kuelewa umuhimu wa kulipia Kodi kwa wakati wameweza kukusanya kiasi cha Tshs millioni 840.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI June 23, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI September 18, 2024
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WOTE December 20, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ELIMU YATOLEWA KWA WAJUMBE WA MABARAZA YA KATA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA

    July 10, 2025
  • WAWAKILISHI WA WAZEE WAKUTANA KWA AJILI YA KUSOMEWA MUONGOZO MPYA WA UANZISHWAJI WA BARAZA LA WAZEE KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA

    July 04, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA YATAKIWA KUTOA ELIMU KWA WAFANYABIASHARA KUHUSIANA NA UUZAJI NA UNUNUZI WA KUTUMIA STAKABADHI GHALANI

    July 02, 2025
  • ZIARA YA MKURUGENZI MTENDAJI YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MAENDELEO YA UJENZI KATIKA HOSPITALI YA WILAYA

    June 27, 2025
  • Angalia zote

Video

Mvamizi wa eneo la soko.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Dira na Dhamira
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Mpango Mkakati
  • Mpango wa Uwekezaji Sekta ya Samaki
  • Muundo wa Taasisi
  • OPRAS - Form

Viunganishi Muambata

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2023 Bundadc
  • Matokeo ya darasa la saba
  • Matokeo ya darasa la saba
  • PO-RALG
  • PO-PSM
  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2019

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Kibara Stoo.

    Anuani ya Posta: 126, Bunda

    Simu: 0282621055

    Hamishika:

    Barua Pepe: ded@bundadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki@ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bunda