Katika kikao cha kamati ya usimamizi na utekelezaji wa mradi wa kuhimili athari za mabadiliko ya Tabianchi (BCRAP), kilichofanyika siku ya tarehe 11/6/2025. Mratibu wa mradi alieleza baadhi ya vipaumbele vitakavyoenda kutekelezwa kwa kipindi cha awamu ya pili ya mradi.
Mratibu wa mradi Ndugu Johaness Bucha alieleza vipaumbele kadhaa ambavyo vitaenda kutekelezwa katika kipindi cha awamu ya pili ya mradi kinachoanzia mwezi wa Saba hadi wa Tisa, 2025.
Ndugu Bucha alisema, katika kipindi cha awamu ya pili, timu ya wataalamu wanaosimamia mradi huo wamepanga kutekeleza zoezi la utoaji wa elimu kwa vikundi ambavyo ni wanufaika wa mradi na kuongeza ufuatiliaji wa Mara kwa mara kuhakikisha vikundi vinatekeleza mradi kama walivyoelekezwa na wataalamu wa mradi, Pia, kuwezesha kuwanunulia vikundi vya kilimo mbegu Bora za zao la Alizeti na kupewa elimu ya usindikaji wa mazao hayo.
Kusimamia utengenezaji na usajili wa katiba ya umoja wa umwagiliaji katika skimu ya mpunga Mchigondo, kuwezesha uanzishwaji na uendelezaji wa vitalu vya miti na matunda, kusambaza na kusimika mizinga ya Nyuki, kusimika miundombinu ya kufikisha maji katika shamba la Mchigondo, ambapo wanatarajia kuanzisha skimu ya umwagiliaji ya Mpunga.
Hivyo, ni baadhi ya vipaumbele ambavyo vinatarajiwa kwenda kutekelezwa katika mradi kwa awamu ya pili.
Naye, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda Ndugu George S Mbilinyi ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya usimamizi na utekelezaji wa mradi alishauri wasimamizi wa utekelezaji wa mradi huo kuhakikisha wanasimamia mradi vizuri ili uwe endelevu katika sekta zote, kuhakikisha wanafuata kanuni, Sheria na taratibu zote za manunuzi kupitia mfumo wa NeST.
Ndugu Mbilinyi aliomba timu nzima kushirikiana kwa pamoja katika kuhakikisha wanatekeleza mradi katika sekta zote na unakuwa endelevu na tija kwa wananchi wote wa Halmashauri ya Bunda.
Mradi wa kuhimili athari za mabadiliko ya Tabianchi unasimamiwa na kutekelezwa na Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, ukifadhiliwa na Mfuko wa Mazingira wa Dunia (Adaptation Fund), chini ya usimamizi wa Baraza la uhifadhi wa mazingira (NEMC).
Kibara Stoo.
Anuani ya Posta: 126, Bunda
Simu: 0282621055
Hamishika:
Barua Pepe: ded@bundadc.go.tz
Haki Miliki@ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bunda