• Malalamiko |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
Bunda District Council
Bunda District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji & Ushirika
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maji
      • Fedha & Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Mifugo & Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi & Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Elimu Msingi
    • Barabara
    • Mifugo
    • Afya
    • Mazao ya kilimo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi & Mipango
      • Elimu, Afya & Maji
      • AIDS Control
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Uma
    • Video
    • Hifadhi ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WALIMU WA SOMO LA HISABATI WA SHULE ZA MSINGI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WANOLEWA

Posted on: November 21st, 2023

Jumla ya Walimu 50 wanaofundisha somo la Hisabati kwa shule za msingi, kutoka Kata 19 zilizopo katika Halmashauri ya wilaya ya Bunda, siku ya tarehe 20/11/2023, walipatiwa mafunzo ya kuwajengea uwezo na mbinu ya kufundisha somo la Hisabati kwa wanafunzi wa shule za Msingi.

Mafunzo hayo yalitolewa na Wakufunzi kutoka chuo cha Ualimu Tarime ambao ni ndugu Ndulu Francis Nkenyenge na ndugu Zacharia Francis Muyembe. Walianza kwa kuwaambia walimu kuunda vikundi ambavyo watajadiliana kwa pamoja kwa kila kundi kuandika matarajio yao wanayotarajia kuyapata baada ya mafunzo hayo.

Mkufunzi Ndulu Francis Nkenyenge, aliwaambia malengo makuu ya mafunzo haya ni kuwawezesha walimu kuchanganua dhana mbalimbali za Hisabati na kuzihusianisha na maisha ya kila siku. Hivyo aliwaambia wawe wanatumia mifano halisi na sio kutoa mifano ambayo haipo katika jamii, yaani mifano ya kusadikika, wanatakiwa watumie mifano halisi ya vitu vinavowazunguka wanafunzi ili wawaelewe.

Ndugu, Nkenyenge pia, aliwaambia walimu wanatakiwa kufundisha kwa ufanisi na umahiri wenye changamoto kwa kutumia mbinu za ufundishaji na dhana stahiki. Pia, wanatakiwa kumudu stadi za upimaji endelevu ili kuboresha ufundishaji wa umahiri wenye changamoto katika ufundishaji.

Baada ya kuelezwa malengo ya mafunzo hayo, Mkufunzi Zacharia Francis Muyembe aliwafundisha umuhimu wa Mafunzo Endelevu Kazini (MEWAKA), kwa kuwataka kuyazingatia kwa umakini kwani yanasaidia kutatua changamoto za ujifunzaji na ufundishaji mahiri mbalimbali.

Alisema mafunzo hayo yanasaidia kuibua mbinu na njia za kufundishia katika mahiri mbalimbali, na pia yanasaidia kuboresha ufundishaji kwa kutumia dhana. Na yanasaidia kufanya tathimini baada ya upimaji, na yanamsaidia Mwalimu kumudu masomo mengine kwa kujifunza.

 Kupitia mafunzo haya walimu waliweza kutambua umuhimu wa MEWAKA na fursa zake katika kuboresha ufundishaji na ujifunzaji wa Hisabati, pia waliweza kubainisha uhusiano wa kimaudhui kati ya moduli ya MEWAKA na muhtasari wa somo la Hisabati kwa darasa la Saba.

Walimu waliwashukuru Wakufunzi kwa mafunzo waliyowapa, pia waliwashukuru, SHULE BORA kwa kuwezesha kufanyika kwa mafunzo haya, na wameomba mafunzo haya yawe endelevu na sio kwa somo la Hisabati peke yake na masomo mengine.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI June 04, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI September 18, 2024
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WOTE December 20, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRATIBU WA MRADI WA BCRAP ATAJA VIPAUMBELE VITAKAVYOENDA KUTEKLELEZWA KWA AWAMU YA PILI YA MRADI

    June 11, 2025
  • ZAIDI YA MILIONI 300 ZA POKELEWA KATIKA UTEKELEZAJI WA MRADI WA KUHIMILI ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIA NCHI

    June 09, 2025
  • ELIMU YA UTUNZAJI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA YATOLEWA KWA WANAFUNZI WA SHULE YA SEKONDARI MWIBARA

    June 04, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    June 03, 2025
  • Angalia zote

Video

Mvamizi wa eneo la soko.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Dira na Dhamira
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Mpango Mkakati
  • Mpango wa Uwekezaji Sekta ya Samaki
  • Muundo wa Taasisi
  • OPRAS - Form

Viunganishi Muambata

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2023 Bundadc
  • Matokeo ya darasa la saba
  • Matokeo ya darasa la saba
  • PO-RALG
  • PO-PSM
  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2019

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Kibara Stoo.

    Anuani ya Posta: 126, Bunda

    Simu: 0282621055

    Hamishika:

    Barua Pepe: ded@bundadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki@ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bunda