Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda Ndugu Oscar J. Nchemwa, ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye maadhimisho ya siku ya wauguzi Duniani, ambapo Halmashauri ya Wilaya ya Bunda iliazimisha siku ya tarehe 30/5/2025, katika kituo cha Afya Ikizu.
Ndugu Nchemwa aliwapongeza wauguzi wote kwa kuadhimisha siku yao Duniani, pia aliwaomba kuendelea kufanya kazi kwa weledi kwa kuzingatia kanuni, Sheria na taratibu za taaluma zao.
" Wauguzi ni watu muhimu sana katika jamii kwani mmekuwa mkifanya kazi muhimu ya kuokoa maisha ya watu, nawapongeza sana na muendelee kuwa na moyo wa huruma wa kuendelea kuwasaidia watu wote bila ubaguzi wowote. Leo hii mmekula kiapo cha kutunza Siri na kufanya kazi kwa moyo mweupe na huruma kwa watu wote, kiapo hiki kikawe silaha yenu muhimu na mkitunze katika kuhakikisha mnatimiza majukumu yenu kwa kufanya kazi kwa weledi mkubwa huku mkizingatia kanuni, Sheria na taratibu za taaluma yenu." Alisema.
Katika risala mliyosoma Leo hii mbali na changamoto mnazokabiliana nazo, nawaomba muendelee kutimiza majukumu yenu na ninawaahidi changamoto zote nimezichukua na ninawaahidi kwenda kuzifanyia kazi kwa kuhakikisha mnakuwa na mazingira rafiki ya kufanya KAZI.
Ndugu Nchemwa alimuagiza Mganga Mkuu wa Halmashauri kuhakikisha anaandaa utaratibu wa kuwapatia wauguzi mafunzo ya kuweza kuingia kwenye mfumo wa PEPMIS ili waweze kujaza majukumu yao, kuhakikisha wauguzi wote wanalipwa stahiki zao kwa wakati ili waweze kufanya kazi.
Katika maadhimisho hayo, Kaimu Mkurugenzi pamoja na wauguzi walitembelea wodi ya wazazi na kutoa zawadi kwa wamama waliolazwa wodini.
Siku ya wauguzi Duniani huadhimishwa kila ifikapo tarehe 12/5 ya Kila mwaka.
Kwa mwaka 2025 siku ya wauguzi Duniani imebeba kauli mbiu isemayo:
" Wauguzi nguvu ya mabadiliko Duniani."
Kibara Stoo.
Anuani ya Posta: 126, Bunda
Simu: 0282621055
Hamishika:
Barua Pepe: ded@bundadc.go.tz
Haki Miliki@ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bunda