Timu ya usimamizi na utekelezaji wa mradi wa kuhimili athari za mabadiliko ya Tabianchi (BCRAP) , imekaa kikao siku ya tarehe 9/6/2025 ikiwa na lengo la kuwasilisha mpangokazi na kujadili namna ya utekelezaji kwa awamu nyingine ya pili.
Mratibu wa mradi Ndugu Johaness Bucha ambaye alikuwa Mwenyekiti wa kikao hicho aliwakaribisha wajumbe wote wanaosimamia na kutekeleza mradi huo ambapo alisema lengo kuu la kuitisha kikao hiki Leo ni kutambulisha mapokezi ya fedha kiasi cha Tshs Million 316 ambazo tumezipokea kwa ajili ya utekelezaji wa mradi kwa kipindi cha awamu ya pili.
Ndugu Bucha aliwataka wajumbe wanaosimamia mradi katika sekta mbalimbali kuhakikisha wanawasilisha mpangokazi wake na kuona ni kwa namna Gani wataenda kutekeleza mradi huo, ambapo wajumbe waliwasilisha mpango kazi katika sekta ya ufugaji, kilimo, uvuvi, maji, wajumbe walijadili kwa kina Kila sekta jinsi itakavyoenda kutekeleza sekta yake kwa kuwataka kuhakikisha wanawafuatilia kwa ukaribu Kila kikundi kuhakikisha wanatekeleza sawa na lengo la mradi lilivyoelekeza ili kuweza kuleta tija kwao na jamii nzima.
" Elimu kwa vikundi ambavyo ni wanufaika wa mradi wa BCRAP iendelee kutolewa ikiwemo usimamizi na utekelezaji wa miradi hiyo, kuhakikisha vikundi vinapewa elimu ya kutosha ya namna ya kutunza akiba kwa kuhakikisha wanakuwa na akaunti katika benki ili ziweze kuwasaidia baade, na sio fedha wanazopata waishie kugawana zote pasipo kuweka akiba ili waweze kuendelea kujiendeleza na kujisimamia wenyewe." Alisisitiza Mratibu.
Aidha, ufuatiliaji wa Mara kwa mara katika vikundi ufanyike ili kuona na kuhakikisha kama wanazingatia mafunzo waliyopewa katika uendelezaji wa miradi yao, wanatekeleza kama walivyoelekezwa na wataalamu.
Pia, Mratibu alishauri kuwepo na ziara ya kuvitembelea vikundi vyote ambavyo viliundwa katika awamu ya kwanza, kuona na kutambua changamoto ambazo wamepitia katika utekelezaji wa mradi kwa awamu ya kwanza na kuwasaidia ili waweze kuendelea kutekeleza na kuendeleza mradi kwa kipindi cha awamu ya pili.
Mradi wa kuhimili athari za mabadliko ya tabianchi, ni mradi unaosimamiwa na kutekelezwa na Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, unafadhiliwa na mfuko wa mazingira wa dunia (Adaptation Fund) chini ya usimamizi wa baraza la Taifa la usimamizi na uhifadhi wa mazingira (NEMC).
See translation
Kibara Stoo.
Anuani ya Posta: 126, Bunda
Simu: 0282621055
Hamishika:
Barua Pepe: ded@bundadc.go.tz
Haki Miliki@ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bunda