• Malalamiko |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
Bunda District Council
Bunda District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji & Ushirika
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maji
      • Fedha & Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Mifugo & Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi & Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Elimu Msingi
    • Barabara
    • Mifugo
    • Afya
    • Mazao ya kilimo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi & Mipango
      • Elimu, Afya & Maji
      • AIDS Control
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Uma
    • Video
    • Hifadhi ya Picha
    • Habari
    • Matukio

ZIARA YA MKURUGENZI MTENDAJI YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MAENDELEO YA UJENZI KATIKA HOSPITALI YA WILAYA

Posted on: June 27th, 2025

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda Ndugu George S Mbilinyi siku ya tarehe 26/6/2025 amefanya ziara ya kutembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa hospitali ya Wilaya iliyopo Kijiji cha Bukama.


Katika ziara hiyo, Ndugu Mbilinyi alitembelea na kukagua ujenzi wa njia za kutembelea wagonjwa, ambao unaendelea kutekelezwa katika hospitali, pia alitembelea na kukagua ukamilishaji wa jengo la wodi ya wanaume, wanawake na watoto.

Aidha, katika ziara hiyo, Ndugu Mbilinyi alitembelea kata ya Salama na kuzungumza na watumishi wote wanaoishi kata ya Salama, lengo kuu la kutembelea kata hiyo ni ufuatiliaji wa maagizo na mikakati waliyopewa kuona kama yametekelezwa kama walivyoagizwa.


Mtendaji wa kata ya Salama, Ndugu Ruben Maduhu aliwasilisha taarifa ya utekelezaji katika Kata, ambapo, aliwasilisha taarifa ya idadi ya majengo yote yaliyopo katika Kata, ambayo yanasifa ya kusajiliwa na yasiyokuwa na sifa ya kusajiliwa kwa ajili ya kuanza kutozwa Kodi.


Pia, aliwasilisha taarifa ya maduka yote yaliyopo katika Kata ya Salama, ambayo yameshakata leseni ya biashara na ambayo hayajakata leseni za biashara, taarifa ya watumishi waliopo katika Kata ya Salama, na taarifa za idara zilitolewa na watumishi husika.


Ndugu Mbilinyi alimuagiza Mtendaji wa Kata kuhakikisha anawasimamia watendaji wote wa vijiji kuhakikisha wanasajili majengo yote yenye sifa katika vijiji na vitongoji vyao ndani ya siku Saba wawe wameshakamilisha na kupata mrejesho.


Kwa upande wa maduka, Ndugu Mbilinyi, alimuagiza Afisa biashara wa Halmashauri Ndugu. Samweli Werema kuhakikisha wanashirikiana na Mtendaji wa kata kuhakikisha hadi ifikapo tarehe 30/6/2025 maduka yote ambayo hayana leseni ya biashara wahakikishe wameshakata na kupata leseni hizo.


" Watumishi wote wanaoishi nje ya maeneo ya kazi, wahakikishe wanahamia na kuishi katika maeneo yao ya kazi". Aliagiza Mkurugenzi Mtendaji.


Taarifa ya idara kilimo katika Kata ya Salama iliwasilishwa na Afisa kilimo, Bi. Experansia Nyaonge., na taarifa ya idara ya Afya iliwasilishwa na Waganga wafawidhi katika zahanati wanazozisimamia.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI June 23, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI September 18, 2024
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WOTE December 20, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ZIARA YA MKURUGENZI MTENDAJI YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MAENDELEO YA UJENZI KATIKA HOSPITALI YA WILAYA

    June 27, 2025
  • BONANZA LA MICHEZO LA WATUMISHI KATI YA HALMASHAURI YA WILAYA YA RORYA, BUNDA DC NA TC

    June 16, 2025
  • MRATIBU WA MRADI WA BCRAP ATAJA VIPAUMBELE VITAKAVYOENDA KUTEKLELEZWA KWA AWAMU YA PILI YA MRADI

    June 11, 2025
  • ZAIDI YA MILIONI 300 ZA POKELEWA KATIKA UTEKELEZAJI WA MRADI WA KUHIMILI ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIA NCHI

    June 09, 2025
  • Angalia zote

Video

Mvamizi wa eneo la soko.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Dira na Dhamira
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Mpango Mkakati
  • Mpango wa Uwekezaji Sekta ya Samaki
  • Muundo wa Taasisi
  • OPRAS - Form

Viunganishi Muambata

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2023 Bundadc
  • Matokeo ya darasa la saba
  • Matokeo ya darasa la saba
  • PO-RALG
  • PO-PSM
  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2019

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Kibara Stoo.

    Anuani ya Posta: 126, Bunda

    Simu: 0282621055

    Hamishika:

    Barua Pepe: ded@bundadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki@ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bunda